Picha ya pamoja na mgeni rasmi na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Maendeleo ya Mazao, Usalama wa Chakula na Ushirika, Dkt. Stephen Nindi baada ya kuzindua mradi wa Dhamana ya Mikopo ya Biashara kwa Sehemu (Partial Trade Credit Guarantee – PCG) kwa ajili ya kuwawezesha wauzaji wadogo wa pembejeo za kilimo kufikisha pembejeo hizo kwa wakulima kwa wakati.
Mgeni rasmi na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Maendeleo ya Mazao, Usalama wa Chakula na Ushirika, Dkt. Stephen Nindi (kushoto) akiwasili katika Ukumbi wa mikutano ndani ya viwanja vya Maonesho ya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma ili kuzindua mradi wa Dhamana ya Mikopo ya Biashara kwa Sehemu (Partial Trade Credit Guarantee – PCG) kwa ajili ya kuwawezesha wauzaji wadogo wa pembejeo za kilimo kufikisha pembejeo hizo kwa wakulima kwa wakati.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Maendeleo ya Mazao, Usalama wa Chakula na Ushirika, Dkt. Stephen Nindi, akizungumza na washiriki wa hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa Dhamana ya Mikopo ya Biashara kwa Sehemu (Partial Trade Credit Guarantee – PCG), katika viwanja vya Maonesho ya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma tarehe 7 Agosti, 2025.
Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA, Joel Laurent, akizungumza na washiriki wa hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa Dhamana ya Mikopo ya Biashara kwa Sehemu (Partial Trade Credit Guarantee – PCG), katika viwanja vya Maonesho ya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma tarehe 7 Agosti, 2025.
Marie Claire Kalihangabo, Mratibu wa Mradi kutoka AFFM, akizungumza na washiriki wa hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa Dhamana ya Mikopo ya Biashara kwa Sehemu (Partial Trade Credit Guarantee – PCG), katika viwanja vya Maonesho ya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma tarehe 7 Agosti, 2025.