Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje, Bi. Nuru Waziri Kindamba, akizungumza na watalaam kutoka Wizara ya Kilimo, Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania na wadau wa tasnia ya mbolea walipofika kutekeleza kampeni ya Mali Shambani Silaha Mbolea tarehe 21 Oktoba, 2025.
Afisa Udhibiti Ubora Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Mushoborozi Christian, akitoa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea wakati wa mafunzo yaliyofanyika katika Kijiji cha Azimio, Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa.
Afisa Udhibiti Ubora Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Chrysanthus Funda, akitoa elimu kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi ya mbolea na upimaji wa afya ya udongo, wakati wa mafunzo yaliyofanyika katika Kijiji cha Katumba, Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa.
Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo, akiwa ameambatana na Sadick Aluwanya, Meneja wa Shamba la Mbegu la ASA lililopo Namtumbo, mkoani Ruvuma, alipowasili katika shamba hilo kujifunza masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na namna wanavyotumia mbolea kwenye uzalishaji wa mbegu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo, akiwa katika picha ya pamoja na watumishi kutoka TFRA, Wakala wa Mbegu Tanzania (ASA) mara baada ya kutembelea shamba la mbegu lililopo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma tarehe 19 Oktoba, 2025. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti wa TFRA, Happiness Mbelle, Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti, na kulia kwake ni Sadick Aluwanya, Meneja wa Shamba la Mbegu la ASA mkoani Ruvuma
Happiness Mbelle, Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) akizungumza na wakulima wa kijiji cha Utili wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma, tarehe 16 Octoba,2025.
Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Kisare makori akizungumza na wadau wa Sekta ya Kilimo(hawapo pichani) walioongozwa na Mkurugenzi wa huduma za Udhibiti wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Hapines Mbelle waliofika kueleza sababu ya kuwepo wilayani humo Tarehe 16 Oktoba, 2025
Wananchi wa kijiji vya Utili na Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, wakifuatilia mafunzo ya matumizi sahihi ya mbolea kutoka kwa wataalam wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), tarehe 16 Oktoba, 2025.