Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Maendeleo ya Mazao, Wizara ya Kilimo, Samson Poneja akizungumza na wakulima wa kijiji cha Mwagwila kilichopo Halmsahuri ya Wilaya Meatu Mkoani Simiyu ikiwa ni utekelezaji wa Kampeni ya Mali Shambani ikilenga kuwaandaa wakulima kutumia pembejeo za kilimo kwa usahihi kuelekea msimu wa kilimo 2025/2026 ili kuongeza tija kwenye uzalishaji tarehe 4 Desemba, 2025
Mkulima wa kijiji cha Mandoya kilichopo Halmsahauri ya Wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu, Kobadi Makoye , akieleza namna anavyotumia mbolea ya samadi katika kilimo cha pamba wakati wa utekelezaji wa kampeni ya Mali shambani unaofanywa baina ya Wizara ya Kilimo na Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), tarehe 4 Desemba , 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha akiwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Wizara ya Kilimo, Idara ya Maendeleo ya Mazao Samson Poneja walipotembelea ofisini kwake kueleza uwepo wao mkoani humo kutekeleza kampeni ya Mali Shambani tarehe 3 Desemba, 2025
Afisa Udhibiti Ubora Mwandamizi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Godwin Vedastus akitoa elimu ya mbolea kwa wakulima wa kijijichi Bukangilija kilichopo Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu leo tarehe 3 Desemba,2025.
Diwani wa Kata ya Sukuma Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, Mary Sagana Misangu ameishukuru Serikali kwa kuwapatia elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo za kilimo wakulima wa kijiji cha Hinduki na kueleza elimu hiyo itawawezesha wakulima kulima kwa tija tarehe 3 Desemba 2025.
Wakulima wa kijiji cha Hinduki kilichopo Halmshauri ya Wilaya ya Maswa Mkoani wa Simiyu wakifuatilia mafunzo ya matumizi sahihi ya mbolea tarehe 3 Desemba, 2025 ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya Mali Shambani yenye lengo la kutoa elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo za kilimo, kuhamasisha wakulima kupima afya ya udongo na kujisajili kwenye mfumo wa pembejeo za kilimo ili kunufaika na ruzuku ya mbolea na mbegu inayotolewa na Serikali.