Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mbugamita kata ya Senani wilayani Maswa wakati wa ziara ya bodi na Menejimenti ya TFRA ya kuhamasisha wakulima kutumia mbolea na kubadilisha uchumi wao kwa kuongeza tija kwenye kilimo chao tarehe 13 Juni, 2025.
Mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), CPA. John Cheyo akizungumza na wakulima wa kijiji cha Mbugamita Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu wakati wa ziara ya bodi na menejimenti ya Mamlaka iliyofanyika tarehe 12 na 13 Juni, 2025 ili kuhamasisha wakulima wa mkoa huo kutumia mbolea kwenye kilimo na kuongeza tija.
aimu Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti TFRA, Bi Elizabeth Bolle akiwahamasisha wakulima wa kijiji cha Mbugamita Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu kulima kisasa kwa kutumia mbolea ili wazalishe kwa tija na kuongeza kipato chao.
Wananchi wa kijiji cha Mbugamita kata ya Senani wilayani Maswa wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo (hayupo pichani) alipokuwa akiwahamasisha kutumia mbolea na kubadilisha mitazamo kuhusu mbolea ili kuongeza tija kwenye kilimo chao tarehe 13 Juni, 2025.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo akizungumza na wakulima wa Chama cha Msingi cha Ushirika wa Wakulima wa Miwa (AMCOS) cha Mkula, Halmashauri ya Ifakara mkoani Morogoro wakati wa ziara iliyolenga kujifunza, kupokea na kutatua changamoto za wakulima hao wa miwa tarehe 26 Mei, 2025.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA, Robert Mtendamema akizungumza mara baada ya kuwasili katika kiwanda cha sukari cha Kilombero mkoani Morogoro tarehe 26 Mei, 2025
Mwenyekiti wa Bodi ya TFRA, Dkt. Anthony Diallo wa pili kutoka kushoto, Dkt. Peter Shimo (kulia) mjumbe wa bodi, Hadija Jabir (kushoto) mjumbe wa bodi na Kaimu Mkurugenzi wa TFRA, Robert Mtendamema (wa kwanza kulia) wakisikiliza maswali ya wakulima Chama cha Msingi cha Ushirika wa Wakulima wa Miwa (AMCOS) cha Mkula, tarehe 26 Mei, 2025 Ifakara mkoani Morogoro
Wanachama wa Chama cha Msingi cha Ushirika wa Wakulima wa Miwa (AMCOS) cha Mkula, Halmashauri ya Wilaya ya Ifakara, mkoani Morogoro, wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo, wakati wa ziara ya kikazi ya Bodi na Menejimenti ya TFRA iliyolenga kujifunza kusikiliza na kutatua changamoto za wakulima hususan katika suala la matumizi sahihi ya mbolea