Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA)

TFRA Logo
TAARIFA KWA UMMA: KUFUNGIWA KUJIHUSISHA NA UUZAJI WA PEMBEJEO ZA KILIMO NCHINI
30 Nov, 2024

TAARIFA KWA UMMA

KUFUNGIWA KUJIHUSISHA NA UUZAJI WA PEMBEJEO ZA KILIMO NCHINI

 

Hivi karibuni, Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) ilifanya ukaguzi na kubaini udanganyifu unaofanywa na baadhi ya kampuni/mawakala wa mbegu na wadau wengine wasio waaminifu wanaouza mbegu zisizothibitishwa ubora na TOSCI. Hali hiyo inaweza kusababisha wakulima kununua mbegu ambazo hazina ubora na kusababisha hasara kwa wakulima na kuhatarisha usalama wa chakula nchini.

Hivyo basi, wafanyabishara wafuatao wamefungiwa kufanya biashara ya mbegu mpaka itakapoamuliwa vinginevyo.

Na

Jina

Namba ya Usajili

Wamiliki/Wakurugenzi

1

Aghahumbi Co. Limited   

SD/663

Omary Mussa Nkwarulo 

Sikujua Issa Kahere

Aghahumbi Omary Nkwarulo

2

Lauria Gwindevya

SD/2426

Lauria L. Gwindevya

 

Vilevile, Wamiliki na Wakurugenzi wa kampuni hizo hawataruhuisiwa kufanya biashara ya pembejeo nchini.

Aidha, kwa kuwa leseni ya biashara ya pembejeo inahusisha mbegu, mbolea na viuatilifu, taarifa inatolewa kwamba usajili/leseni zilizotolewa kwa kampuni hizo na Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) zimefungiwa kwa kipindi chote cha utekelezaji wa agizo hili.

Taarifa za kufungiwa kwa kampuni hizi zitawasilishwa pia kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa ili zifutiwe leseni zao za biashara.

Kupitia tangazo hili, waagizaji, wazalishaji na wasambazaji wa pembejeo wanakumbushwa kutojihusisha na udanganyifu wa aina yoyote ili kuepuka mkono wa  sheria  ikiwa ni pamoja na kufutiwa hati za usajili/leseni ya kufanya biashara zinazohusiana na uuzaji na usambazaji wa pembejeo za kilimo nchini.

Pakuwa Taarifa kwa Umma Hapa

Imetolewa tarehe 30/11/2024  kwa idhini ya:

 

                                              Mkurugenzi Mkuu                 Mkurugenzi Mtendaji                     Mkurugenzi Mkuu

                                                        TOSCI                                      TFRA                                          TPHPA

Kwa taarifa zaidi:

Tembelea ofisi za TOSCI Morogoro.