Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka 2025/2026 ya shilingi trilioni 1.24 leo tarehe 21 Mei 2025, Bungeni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ndc. Gerald Mweli (wa kwanza kushoto) na Naibu Katibu Mkuu anayesimamia Ushirika na Umwagiliaji, Dkt, Stephen Nindi wakifuatailia uwasilishaji wa bajeti ya Wizara ya Kilimo ya mwaka wa fedha 2025/2026.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania , TFRA (katikati) Joel Laurent akifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa Hotuba ya Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Mohamed Bashe (Mb), kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya
Kilimo kwa mwaka 2025/26 Bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 21Mei, 2025.