Wakati wa ziara ya kukagua maghala ya waagizaji wa mbolea jijini Dar es salaam , Mhe. Chongolo amesema kampuni ya ETG Inputs Ltd pekee ina zaidi ya tani 47,000 za mbolea ambazo tayari zimesambazwa katika maeneo mbalimbali ya nchi yakiwemo Mbeya, Iringa na Kilimanjaro, huku gari zikiendelea kupelekwa katika mikoa mingine kulingana na mahitaji ya wakulima.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb), amewahakikishia wakulima nchini kuwa mbolea inapatikana kwa wingi na hakuna sababu ya kuwa na hofu kuhusu upatikanaji wake katika msimu unaoendelea wa kilimo na msimu ujao.
Ghala la mbolea litakalo hudumia mikoa ya kusini mwa Tanzania
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania, Joel Laurent wakati wa uzinduzi wa ghala la mbolea litakalo hudumia mikoa ya kusini mwa Tanzania tarehe 25 Mei, 2026.
Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo(Mb) akizugumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania, Joel Laurent wakati wa uzinduzi wa ghala la mbolea litakalo hudumia mikoa ya kusini mwa Tanzania tarehe 25 Mei, 2026.