Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibi wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent akizungumza jambo alipotembelea banda la Mamlalaka katika maonesho ya biashara ya kimataifa ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam tar 10/7/2025.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibi wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent (kulia) akimsikiliza Meneja wa Uhusiano, Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa TFRA, Bi. Matilda Kasanga (kulia) alipotembelea banda la Mamlalaka hiyo katika maonesho ya biashara ya kimataifa ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam tar 10/7/2025.
Mjumbe wa bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania ( TFRA), Dkt. Peter Shimo akiwa katika picha na watumishi wa TFRA mara baada kutembelea Banda la Mamlaka katika maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara (SABASABA) yanayoendelea jijini Dar es Salaam tarehe 5 Julai 2025.
Mjumbe wa Bodi ya TFRA, Dkt. Peter Shimo akipokea maelezo kutoka kwa mtafiti wa Kilimo wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI), Mgaya Maumba alipotembelea banda hilo wakati wa maonesho ya 49 ya biashara ya Kimataifa (SABASABA) tarehe 5 Julai, 2025
Mwakilishi wa Mbolea za Ruzuku Mkoa wa Dar es Salaam, Claudia Morandi, akitoa elimu ya Mbolea kwa mwanachi aliyembelea Banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania(TFRA) katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara( SABASABA) jijini Dar es Salaam, tarehe 1 Julai, 2025.
TFRA washiriki maonyesho ya biashara ya kimataifa Sabasaba 2025
Mtaalamu wa Maabara wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania(TFRA), Oscar Comred akitoa elimu ya mbolea kwa mwananchi katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara (SABASABA) yanayofanyika jijini Dar es Salaam, tarehe 1 Julai,2025.
TFRA washiriki maonyesho ya biashara ya kimataifa Sabasaba 2025