Mkutano wa Mbolea Afrikaa Argus 2026 unawakutanisha watunga sera, wawekezaji, wasafirishaji, wazalishaji na wadau wa sekta ya mbolea kutoka Afrika na nje ya bara, ukilenga kujadili fursa za uwekezaji, kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kuweka mikakati, kuhakikisha upatikanaji wa mbolea bora na kwa gharama nafuu ili kuchochea maendeleo ya kilimo na usalama wa chakula.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Joel Laurent, amesema Tanzania ni miongoni mwa masoko ya mbolea yanayokua kwa kasi zaidi barani Afrika, na kuchochea matumizi ya mbolea kutoka tani 360,000 mwaka 2021/2022 hadi takribani tani milioni moja kwa mwaka 2024/2025, huku matarajio yakionesha mahitaji kufikia tani milioni 2.1 ifikapo mwaka 2030.