Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA)

TFRA Logo
MAFUNZO YA BIASHARA YA MBOLEA –MKOA WA IRINGA MJINI, UKUMBI WA UMAKI, TAREHE 27 NA 28 AGOSTI 2026: OFISI YA TFRA DODOMA IMEANDAA
19 Aug, 2026

MAFUNZO YA BIASHARA YA MBOLEA – IRINGA MJINI

Ofisi ya TFRA Dodoma inawatangazia na kuwakaribisha wadau wote kushiriki katika Mafunzo ya Biashara ya Mbolea yatakayofanyika:

📍 Mahali: Ukumbi wa UMAKI, Iringa Mjini
📅 Tarehe: 27 na 28 Agosti 2026
🕑 Muda: Saa 2:00 Asubuhi

Mafunzo haya yanawalenga:

  • Wanaotaka kuanzisha biashara ya mbolea

  • Wafanyabiashara wa mbolea

  • Vyama vya Ushirika

  • Wafanyakazi wa maduka ya mbolea

  • Wafanyakazi wa maghala ya mbolea

Tunawakaribisha wote kujifunza kuhusu taratibu, kanuni na mahitaji muhimu ya kuanzisha na kuendesha biashara ya mbolea kwa usahihi.

OFISI YA TFRA DODOMA

Karibu ujifunze, uelewe na uanzishe biashara sahihi ya mbolea!