Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA)

TFRA Logo
Kiongozi wa mbio za Mwenge 2026 aipa heko TFRA Kwa kuwashika mkono vijana
22 May, 2026
Kiongozi wa mbio za Mwenge 2026 aipa heko TFRA Kwa kuwashika mkono vijana

Kiongozi wa mbio za Mwenge 2026 aipa heko TFRA Kwa kuwashika mkono vijana

Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2026, Wazo  Mwang'onda ameipongeza Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea  Tanzania (TFRA) kwa kuwasaidia vijana zaidi ya 160 kwa kuwapatia mbolea  ambayo  imewaletea tija shambani, huku akiomba waendelea kuwasaidia zaidi kwa kuwapa elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo hiyo muhimu ili wafanye kilimo chenye tija ambacho kitawainua kiuchumi. 

Mwang'onda ameyasema hayo  baada ya kutembelea na kukagua banda la TFRA katika eneo la mkesha wa mwenge wilayani makete, na kuwasihi wataalamu kutoka Mamlaka hiyo kujikita zaidi kuwasaidia vijana ili waweze kuinuka kichumi. 

Aidha,ameeleza kuwa vijana ndio nguvu kazi pekee inayoweza kuleta mabadiliko nchini kupitia sekta ya kilimo iwapo watapewa elimu sahihi ya kufanya kilimo chenye tija ambacho kitaleta matokeo ya wazi. 

Naye Afisa Udhibiti Ubora  TFRA Nyanda za Juu Kusini,  Chrisantus Funda amesema Mamlaka itaendelea kuwasaidia vijana kwa kutoa elimu stahiki  na kuwasogeza karibu kwa uangalizi kupitia maafisa kilimo wa wilaya ili wengi wajikite katika sekta ya kilimo itakayowasaidia kuinuka kichumi na kupunguza wimbi la vijana wasio na Ajira nchini. 

"Ikumbukwe kwamba TFRA imekuwa sehemu ya kuwasaidia vijana katika sekta ya kilimo baada ya kutoa mifuko zaidi ya 200 ya mbolea kupitia  programu iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Makete  Kissa Kasongwa ambayo inewanufaisha vijana wengi. 

Aidha,  Funda amemshukuru  kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Wazo Michael Mwang'onda kwa kutambua juhudi za TFRA kwa kuendelea kuwa karibu na wakulima hususani maeneo ya vijijini na kusimamia upatikanaji wa mbolea.