Wafanyabiashara wa mbolea waondolewa hofu mizigo kucheleweshwa bandarini
29 May, 2024

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Stephan Ngailo akiambatana na wafanyabiashara wa mbolea nchini wamekutana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), Eric Hamissi kujadili namna bora ya kutatua changamoto wanazokutana nazo wafanyabiashara hao nchini.
Kikao hicho kilifanyika jana tarehe 18 Machi, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa bandari Jijini Dar es Salaam na kufikia mwisho mzuri baada ya wafanyabiashara kuondolewa wasiwasi wa mizigo yao kuchelewa kupakuliwa katika bandari hiyo kufuatia juhudi shirikishi baina ya TFRA, TPA na wafanyabiashara wa mbolea.